Description
Kwa hakika miongoni mwa mambo ambayo humpata binadamu mara kwa mara ni maradhi, na bila shaka mwanadamu mpaka sasa ameshatumia juhudi kubwa ili kuponya maradhi hayo au kupunguza athari zake mbaya, hivyo amefungua hospitali nyingi na vituo vya afya chungu nzima, na ametenga vitivo mahusi vya masomo ya tiba na uchunguzi wa magonjwa mbalimbali, aidha pia ametumia fedha nyingi ili kushughulikia suala la upunguzaji wa athari na maumivu ya maradhi husika.