Description
Afya ya mwili kwa mwanadamu ni kitu muhimu sana. lli mwanadamu aweze kuyajenga maisha yake na kuwa bora kimwili, lazima awe na afya bora, na sio tu kwa ajili ya kuendesha maisha yake, bali pia bila afya nzuri mtu hawezi kutekeleza ibada zake sawasawa jinsi inavyotakiwa kuifanya. Hivyo, kama Uislamu ulivyo kwamba ni dini na ni mfumo kamili wa maisha, umeelezea kwa kina huduma ya afya, yaani mtu akiwa nini ili ajipatie afya njema.